Watu watano wameuwawa na wengine
watano kujeruhiwa katika tukio la shambulizi la kutumia risasi katika
mkoa wa kusini mwa China wa Hebei.
Mtu mwenye silaha Liu Shuangrui
anayedaiwa kufanya mauaji hayo ameuwawa, ambapo pia imeelezwa
miongoni mwa waliouwawa wamo maafisa polisi wawili na watu wengine
kujeruhiwa.
Matukio ya mauaji ya kutumia silaha
ni nadra kutokea nchini China, kutokana na kuwa na sheria kali za
udhibiti wa umiliki wa silaha.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni