Nchi ya Chad imepiga marufuku watu
kuvaa vazi la kufunika sura yote, kufuatia matukio mawili ya mabomu
ya kujitoa mhanga yaliyotokea siku ya jumatatu.
Serikali ya Chad inalituhumu kundi
la wapiganaji wa Boko Haram kwa kuhusika na milipuko hiyo ambayo
imeuwa zaidi ya watu 20.
Waziri Mkuu wa nchi hiyo amesema
vazi la kufunika sura yote lilitumika kujifichia wapiganaji wa kundi
hilo na kusema maafisa usalama watachomamoto mavazi ya kufunika
sura yote.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni