.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 28 Juni 2015

WAANDAJI WA SHEREHE ILIYOJERUHI WATU 500 WAKAMATWA NA KUHOJIWA NCHINI TAIWANI

Waandaaji wa sherehe katika uwanja wa wazi nchini Taiwani wamekamatwa na vyombo vya dola vya nchi hiyo na kuhojiwa baada ya moto kulipuka kati kati ya mkusanyiko wa watu waliohudhuria sherehe hiyo.

Watu zaidi ya 500 walimejeruhiwa kufuatia tukio hilo, kufuatia poda yenye rangi kuwaka moto baada ya kurushwa na mtammbo uliokuwa kwenye jukwaa kuelekea kwenye mkusanyiko wa watu.

Picha zilizopigwa zinaonyesha watu wakiwa wamechanganyikiwa na kupiga mayowe ambapo maboya ya kulalia ya kujaza kwa upepo yalitumika kama machela za kubebea majeruhi. Kufuatia tukio hilo watu 182 wamelazwa kwenye chumba cha wagonjwa mahututi.
                     Watu waliokuwepo kwenye sherehe hiyo wakilia kwa uchungu

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni