Ripoti ya Umoja wa Mataifa imesema
walinda amani wa umoja huo wamekuwa wakibadilishana bidhaa na huduma
ya ngono kwa watu ambao chombo hicho kimekuwa kikifanyakazi ya
kusaidia wananchi.
Taarifa ya Ofisi ya Umoja wa
Mataifa, inayoangalia huduma zake (OIOS) imebaini kuwa mamia ya
wanawake katika nchi za Haiti na Liberia wamelazimika kujiuza miili
yao kutokana na njaa na umasikini.
Wanawake hao wamekuwa wakilipwa
fedha, vito vya thamani, simu pamoja na bidhaa nyingine na walinda
amani wa Umoja wa Mataifa, na kulazimika kufanya nao ngono.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni