Watalii wanne waliovua nguo na
kupiga picha wakiwa juu ya mlima mtakatifu nchini Malaysia wamepatiwa
kifungo cha jela cha siku tatu pamoja na faini.
Watalii hao Muingereza Eleanor
Hawkins, raia wa Canada Lindsey na Danielle Peterson pamoja na
Mholanzi Dylan Snel wametiwa hatiani kwa kusababisha kero kwa umma.
Kundi hilo la watalii linatuhumiwa
kuwa kitendo chao hicho ndicho kilichosababisha kutokea kwa tetemeko
la ardhi, baada ya kupiga picha na nguo za ndani juu ya Mlima
Kinabalu.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni