.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 27 Julai 2015

MAKABURI SITA YALIYOZIKWA WATU WENGI YAMEBAINIKA NCHINI MEXICO

Makaburi sita yaliyozikwa watu wengi yamebainika kusini mwa jimbo la Guerrero nchini Mexico, wakati wa msako wa wanafunzi 43 wa ualimu waliotekwa mwezi Septemba mwaka jana.

Ofisi ya Mwanasheria Mkuu imesema mabaki ya miili 129, imebainika kutoka kwenye makaburi hayo.

Hata hivyo hakuna hata mwili mmoja wa mabaki hayo, uliohusishwa na wanafunzi hao 43 ambao hawajulikani iwapo wapo hai ama wamekufa tangu watekwe eneo la Iguala.

Kwa mujibu wa taarifa, kati ya miili 129 iliyokutwa kwenye makaburi hayo, 112 ni ya wanaume, 20 wanawake na wengine waliobakia hawajatambulika jinsia zao.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni