.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 28 Julai 2015

RAIS WA FFB KUWASILI LEO

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini Burundu (FFB), Reverien Ndikuriyo anatarajiwa kuwasili leo saa 5 usiku jijini Dar es salaam kwa shirika la Ndege la Rwanda Air.

Ndikuriyo anatarjaiwa kuwa na mazungumzo na Rais wa TFF, Jamali Malinzi kisha atashuhudia michuano ya kombe la Kagame inayoendelea kutimua vumbi jijini Dar es salaam ikiwa katika hatua ya robo fainali kwa sasa.

Aidha Vicent Nzamwita Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini Rwanda (FERWAFA) anatarajiwa kuwasili nchini alhamis akiambatana na kocha wa timu ya Taifa ya Rwanda (Amavubi) John McKinstry.

Rais wa FERWAFA anatarajiwa kuwa na mazungumzo na Rais wa TFF, Jamal Malinzi na baadae kuhudhuria michuano ya Kombe la Kagame inayoendelea nchini Tanzania.

IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni