.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 28 Julai 2015

RAIS YOWERI MUSEVENI ATOA FEDHA KUCHANGIA JENGO LA WASANII UGANDA

Rais Yoweri Museveni wa Uganda amechangia kiasi cha shilingi milioni 400 katika ujenzi wa jengo la ofisi zitakazotumiwa na wasanii wa nchini Uganda.

Museveni ni mpenzi wa muziki na aliachia wimbo wake wa 'Mpenkoni' miaka mitano iliyopita na hivi karibuni ameachia wimbo wa 'Yengoma' kwenye You Tube ambao umepata watu 6,100 na kupakuliwa mara 7,500 hadi kufikia mwishoni mwa wiki iliyoisha.

Rais Museveni ametangaza mchango wake huo wa fedha baada ya wasanii wa muziki na sanaa kumuomba kuwatafutia eneo la ardhi kwa ajili ya kujenga jengo la makao makuu ya wasanii nchini Uganda.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni