.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 6 Julai 2015

WAZIRI MKUU WA UGIRIKI ALEXIS TSIPRAS AWAPONGEZA WANANCHI KWA KUPIGA KURA YA HAPANA

Waziri Mkuu wa Ugiriki Alexis Tsipras, amesema wananchi wa taifa hilo wamefanya uamuzi wa busara kwa kupiga kura ya kupinga masharti ya kimatiafa ya kuisaidia kuikomboa kiuchumi.

Matokeo ya mwisho ya kura ya maoni yanaonyesha asilimia 61.3 ya wananchi wa Ugiriki wamekataa masharti ya kimataifa na asilimia 38.7 wameridhia masharti.

Maelfu ya wananchi wa Ugiriki wamekuwa wakisherehekea uamuzi huo mitaani wakipeperusha bendera, wakipaza sauti zao na kufyatua fashifashi.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni