.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 11 Agosti 2015

BARAZA LA USALAMA UN LAISHINIKIZA SERIKALI YA BURUNDI KUZUNGUMZA NA UPINZANI

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa (UN), limeishinikiza serikali ya Burundi kuanzisha mara moja mazungumzo na upinzania ili kukomesha ghasia zinazoelekea kuitumbukiza nchi hiyo kwenye machafuko.

Wajumbe 15 wa baraza hilo wakiungwa mkono na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Ban Ki-moon wametuma ujumbe wa ngazi ya juu wa umoja huo kujaribu kutuliza mgogoro wa Burundi.

Baraza hilo limetaka kuwepo mazungumzo baada ya maafisa waandamizi wa UN kuonya katika mkutano wa ndani wa dharura ulioitishwa na Ufaransa kuwa machafuko yanazidi kukithiri katika nchi ya Burundi.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni