.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 18 Agosti 2015

BARUA PEPE 300 ZA BI. HILLARY CLINTON KUPITIWA KWA UCHUNGUZI

Zaidi ya barua pepe 300 kutoka katika seva binafsi ya Bi. Hillary Clinton zitapitiwa kubaini iwapo zilikuwa na taarifa za siri za serikali.

Idara ya serikali ya Marekani ilibaini barua pepe hizo na inaangalia iwapo zinaweza kutolewa kwa umma.

Bi. Clinton alitumia mail ya binafsi akiwa waziri wa mambo ya nje katika miaka minne na kuibua wimbi la kumkosoa kwa kwenda kinyume na taratibu za serikali.

Hata hivyo Bi. Clinton anayewania urais kwa tiketi ya chama cha Democratic mwakani amesema email yake haikuwa na nyaraka za siri za serikali kwa wakati huo.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni