.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 6 Agosti 2015

BOTI ILIYOZAMA LIBYA MATUMANI YA KUWAPATA MANUSURA ZAIDI YATOWEKA

Waokoaji wanaotafuta manusura wa ajali ya boti iliyozama bahari ya Mediterranean ikiwa na wahamiaji 600 kutoka Afrika katika Pwani ya Libya wameondoa matumaini ya kupata watu walio hai.

Maafisa hao awali walihofia kuwa mamia ya wahamiaji hao watakuwa wamekufa maji, hata hivyo Shirika la Kuwahudumia Wakimbizi Duniani, UNHCR limesema watu 400 wameokolewa.

Walinzi wa Pwani ya Italia wameeleza kuwa miili 25 imepatikana hadi sasa hata hivyo haijulikani ni idadi gani ya watu ambao bado hawajapatikana.

Zaidi ya wahamiaji 2,000 inasemekana wamekufa katika mwaka 2015 wakijaribu kukatiza baharia ya Mediterranean kwenda Ulaya.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni