Kundi la 'Majoker Crew' wakiingia
stejini kwa namna ya pekee kabisaa.
Majaji wakiendelea na shughuli yao
ya kupima uwezo kukokotoa na kutoa alama kwa madansa.
Kundi la 'The Winners Crew'
wakionyesha makali yao kwa steji.
Mashabiki wakifuatilia mashindano
kwa makini.
Mashindano ya Dance 100% 2015 hatua
ya Robo Fainali hatimae yamekamilika na kufanikisha kupatikana kwa
makundi 10 ambayo yanasonga mbele kulekea hatua ya fainali ya
mashindano hayo makubwa Afrika Mashariki.
Kutokana na uwezo mkubwa
walioonyesha mbele ya majaji Majokery, Wazawa Crew, The Best, Cute
Babies, Best Boys Kaka Zao, The Winners, Team ya Shamba, The WD, Team
Makorokocho na Quality Boys ndio makundi yaliyofanikiwa kuingia nusu
fainali.
Upekee na mvuto wa aina yake kutoka
kwa mashabiki kati ya mambo mengine ulikuwa ni muonekano mpya ya set
ya Jukwaa la madansa jipya kabisa ambalo lipo juu lililowezesha kila
aliyeweza kufika kujionea burudani ya dansi na ubunifu katika hali ya
kipekee.
Kwa kipekee pia na kwa tathmini ya
majaji, Kundi la Majokery ni kati ya washindano waliomwagiwa sifa
nyingi kwa kuzingatia kuhusisha nyimbo za kitamaduni katika dansi
yao, na vilevile usimuliaji wa hadithi kupitia kile walichokicheza.
Kama sehemu ya Tathmini ya
mashindano hayo, Mratibu wa mashindano kutoka BASATA, Kwerugira
Maregesi ametoa wito kwa makundi yaliyofanikiwa kuingia nusu fainali
kuongeza mazoezi zaidi na kuzingatia vigezo vya mashindano kama siri
pekee ya kuweza kushinda.
Mpango huo mzima ambao ulisimamiwa
vizuri na majaji Super Nyamwela, Queen Darleen na Shetta na
kushereheshwa na T Bway pamoja na Maggie Vampire, umeletwa kwako na
team nzima ya East Africa Radio na East Africa TV na kudhaminiwa kwa
nguvu kabisa na Coca Cola na Vodacom Tanzania.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni