.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 18 Agosti 2015

KENYA YATANGAZA MAJINA YA WANAOSHAWISHI VIJANA KUJIUNGA NA MAGAIDI

Polisi nchini Kenya wamewataja wanaume watatu ambao wanadai kuwa wamekuwa wakihusika na kuwaandikisha vijana kujiunga na vikundi vya ugaidi.

Watu hao Abdifatah Abubakar Ahmed, Ramadhan Hamisi Kufungwa na Ahmed Imam Ali ingawa awali walikuwa wakifanya shughuli zao Kenya, hivi sasa wamekimbilia nchini Somalia ambayo ni kitovu cha ugaidi.

Watuhumiwa hao watiifu wa kundi la Al Shabaab wametuhumiwa kwa kuwashawishi vijana kwa njia ya intaneti wakiwemo wa vyuo vikuu, kwa kuwaahidi fedha nyingi pamoja na mambo mengine mazuri.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni