.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 14 Agosti 2015

MARUBANI WAKOSA HEWA WAKIWA ANGANI NA KULAZIMIKA KUTUA KWA DHARURA

Marubani wa ndege ya British Airways iliyokuwa inaenda Marekani ikiwa na abiria 221 wameugua hafla wakiwa futi 10,000 angani na kulazimika kutua kwa dharura baada ya njia za viyoyozi vya chumba chao kuziba.

Marubani watatu walilazimika kutumia masks za kupitishia hewa ya oxygeni, ili kuweza kutua tena Jijini London baada ya kusafiri kwa saa moja.

Baada ya uchunguzi ilibainika kuwa njia za viyoyozi katika chumba cha marubaini zilikuwa zimezibwa na vipande vya waya, karatasi za kufungia nyaya pamoja na vitu vingine.

Marubani hao watatu walianza kusikia kuumwa kichwa na kizunguzungu ndipo walipovuta masks za hewa ya oxygeni na kuomba kutua kwa dharura.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni