.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 19 Agosti 2015

MEMPHIS DEPAY AIBEBA MANCHESTER UNITED KWA KUTUNDIKA MABAO MAWILI

Mchezaji mpya wa Manchester United, Memphis Depay aliyenunuliwa kwa paundi milioni 30, ameanza kuonyesha makali yake baada ya jana kuifungia timu yake mabao mawili dhidi ya Klabu ya Brugge katika mchezo wa Ligi ya Mabigwa kuwania kuingia hatua ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.

Timu ya Brugge ilikuwa ya kwanza kuiamsha Manchester United baada ya kupata goli la kujifunga Michael Carrick kufuatia mpira wa adhabu, lakini Depay alisawazisha kwa shuti la chini la kuzungusha mpira umbali wa yadi 25.

Depay kama haitoshi alifunga bao la pili kwa shuti la kuzungusha mpira wa juu na kisha kumpigia krosi ya pande la kichwa Marouane Fellaini aliyetikisa nyavu na kuiandikia Manchester united bao la tatu.
 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni