Mwanaume mmoja wa Morocco amekufa
kwa kukosa hewa akiwa kwenye sanduku wakati kaka yake akijaribu
kumsafirisha kimagendo kwenye buti la gari yake kuelekea Hispania.
Mwanaume huyo mwenye umri wa miaka
27, alikuwa kwenye kivuko kutoka eneo la Afrika ya Kaskazini Melila
kuelekea Hispania katika mji wa Almeria.
Kaka wa mwanaume huyo ambaye
anamiliki hati ya kusafiri ya Ufaransa amefunguliwa mashtaka ya kuua
bila ya kukusudia.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni