Mwanaharakati mashuhuri nchini
Burundi amepigwa risasi na kujeruhiwa vibaya na mtu mwenye silaha
aliyekuwa kwenye pikipiki.
Kwa mujibu wa familia yake
mwanaharakati huyo Claver Mbonimpa ameshambuliwa katika Jiji la
Bujumbura.
Mwanaharakati huyo ni miongoni mwa
wakosoaji wakubwa wa rais Pierre Nkurunziza katika uamuzi wake wa
kuwania urais kwa muhula wa tatu.
Siku ya jumapili msaidizi wa rais
Jenerali, Adolphe Nshimirimana aliuwawa kwa kushambuliwa kwa risasi
Jijini Bujumbura.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni