Naibu Waziri wa Kazi na Ajira ambaye
pia ni Mbunge wa CCM jimbo la Segerea anayemaliza muda wake, Dkt.
Milton Makongoro Mahanga ametangaza rasmi kujiunga na Chama cha
Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
Dkt. Mahanga ametangaza uamuzi huo
leo mbele ya waandishi wa habari akiwa nyumbani kwake Segerea mwisho,
ambapo amesema ameamua kuachana na Chama cha Mapinduzi (CCM) na
kujiunga na (CHADEMA).
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni