Afrika Kusini imewatia hatiani
polisi wanane kwa kumuua dereva taksi raia wa Msumbiji, ambaye
alifungwa nyuma ya gari na kuburuzwa barabarani mwaka 2013.
Jaji amesema kuwa hakuna shaka kuwa
polisi walijua kuwa kitendo chao hicho kinaweza kusababisha kifo cha
mtu huyo Mido Macia.
Makundi ya kutetea haki za binadamu
mara kwa mara yamekuwa yakishutumu polisi nchini Afrika Kusini kwa
ukatili.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni