.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 5 Agosti 2015

PROF. IBRAHIM LIPUMBA AHAIRISHA KUKUTANA NA WAANDISHI WA HABARI

Mkutano wa waandishi wa habari na Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF, Prof. Ibrahim Lipumba ambao aliutisha ili kutoa tamko lake umeahirishwa hii leo kutokana na kuwa na kikao na wazee wa chama hicho kabla ya kuongea na waandishi.

Akizungumza katika ofisi za chama hicho Jijini Dar es Salaam Naibu Katibu Mkuu wa CUF, Bi. Magdalena Sakaya amesema kuwa wamelazimika kuahirisha mkutano huo kutokana na kikao kirefu baina ya Prof. Lipumba na wazee hao ambao wametaka kujua anataka kutoa tamko gani kwa waandishi wa habari.

Kufuatia kauli hiyo waandishi wa habari walilazimika kuondoka katika eneo la ofisi hizo huku baadhi ya wanachama wa CUF, wakiendelea kuwepo nje ya ofisi zao wakidai wanangojea kumuona Prof. Lipumba japo hata awasalimie baada ya kumaliza kikao hicho.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni