.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 10 Agosti 2015

UTURUKI YAKUMBWA NA MASHAMBULIZI YA MFULULIZO HII LEO

Wimbi la mashambulizi limeikumba nchi ya Uturuki hii leo, ambapo maafisa polisi wanne wameuwawa kusini mashariki mwa nchi hiyo huku mlipuko wa bomu ukitokea katika Jiji la Istanbul.

Kwa nyakati tofauti, washambuliaji wawili wenye silaha walifyatua risasi nje ya ofisi ndogo ya Ubalozi wa Marekani huko Istanbul, hata hivyo hakuna hata mtu mmoja aliyejeruhiwa.

Maafisa polisi wanne wameuwawa kwa mlipuko katika barabara ya mkoa wa Sirnak, muda mfupi tu baada ya wapiganaji kufyatulia risasi helkopta ya jeshi na kumuua mwanajeshi mmoja.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni