.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 19 Agosti 2015

WAGONJWA WA KIPINDUPINDU DAR WAONGEZEKA NA KUFIKIA 40

Ugonjwa wa kipindupindu umezidi kushika kasi Jijini Dar es Salaam tangu kutokea mlipuko wake mwishoni mwa wiki iliyopita ambapo sasa idadi ya wagonjwa imeongezeka kutoka wagonjwa 36 jana na kufikia wagonjwa 40 leo.

Kufuatia hali hiyo Mganga Mkuu wa Manispaa ya Kinondoni Bw. Aziz Msuya amesema manispaa hiyo imeanza zoezi la kuwaondoa wauza vyakula vya kupikwa wanaouza vyakula vyao karibu na maeneo yanayotiririka maji machafu.

Aidha, Bw. Aziz amewataka wananchi kumuwahisha hospitali mara moja mgonjwa yeyote ambaye atabainika kutapika na kuharisha mfululizo ili aweze kupatiwa matibabu ya haraka.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni