Katibu Mkuu
Umoja wa Mataifa Bw. Ban Ki-moon ameshutumu vikali shambulio la
jumapili lililofanywa kwa walinda amani huko Darfur ambalo
lilisababisha kifo cha mwanajeshi wa Afrika Kusini.
Katika taarifa
yake Bw. Ki-moon ametoa salamu za rambirambi zake kwa serikali ya
Afrika Kusini na watu wake pamoja na familia ya mlinda amani huyo
aliyekufa.
Pia Katibu Mkuu
huyo wa Umoja wa Mataifa amewatakia wapone haraka wanajeshi
waliojeruhiwa katika tukio hilo.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni