Barcelona imepata kipigo kikubwa
katika ligi ya La Liga tangu inolewe na Luis Enrique wakati timu
Celta Vigo ikikatisha rekodi ya ushindi wa asilimia 100 katika msimu
huu kwa kuifunga mbao 4-1.
Mshambuliaji wa zamani wa Liverpool
Iago Aspas alipachika wavuni mabao mawili baada ya Nolito kufunga
bao la kwanza dhidi ya timu yake ya zamani ya Barcelona.
Neymar alipachika bao moja la
kufutia machozi kwa Barcelona zikiwa zimebakia dakika10 za mchezo
huo, kabla ya mchezaji wa zamani wa Manchester City na Stoke John Guidetti kufunga
bao la nne la Celta Vigo.
John Guidetti akifunga
bao la nne la Celta Vigo
Lionel Messi akiwa ameshika kiuno hoi kwa kipigo



Hakuna maoni :
Chapisha Maoni