Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya
Dangote, Alhaj Aliko Dangote (aliyesimama katikati), akizungumza na
maofisa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Wizara ya Mambo y Nje, Viwanda
na Biashara na Masoko, Kituo cha Uwekezaji Tanznia (TIC) na taasisi
mbalimbali za serikali, walipokutana na Mtendaji huyo mkoani Mtwara
jana kujadili kuhusu uzinduzi wa kiwanda hicho kikubwa cha simenti.
Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya
Dangote, Alhaj Aliko Dangote (kushoto), akiwasikiliza kwa makini
maofisa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje, Viwanda,
Biashara na Masoko na Kituo cha Uwekezaji Tanzani (TIC),
waliotembelea kiwanda cha simenti cha Dangote kinachojengwa mkoani
Mtwara jana kwa ajili ya maandalizi ya kuzindua rasmi Oktoba mwaka
huu.
Mwekezaji kutoka Nigeria, Mtendaji
Mkuu wa Makampuni ya Dangote, Alhaj Aliko Dangote (kushoto),
akiwasikiliza kwa makini Mkurugenzi wa Dangote Makao Makuu, Bw. Sada
Ladan Baki (kulia), Mwakilishi Mkazi wa Makampuni hayo, Bi. Esther
Baruti na Kaimu Balozi wa Nigeria, Bw. S. Umaru, alipokutana nao
kwenye mradi mkubwa wa ujenzi wa kiwanda cha simenti mkoani Mtwara
jana.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni