Watu sita akiwemo mwanamke mjamzito
wamekufa baada ya gari kuteleza na kuacha barabara wakati wa mbio za
magari kaskazini magharibi mwa Hispania.
Polisi wamesema watu 16 wamejeruhiwa
katika tukio hilo, baadhi yao wakiwa mahututi baada ya kutokea ajali
hiyo katika mbio za magari za A Coruna.
Picha za video zinaonyesha gari
likiacha barabara na kuwagonga watu waliokuwa wakifuatilia mbio hizo
kando ya barabara. Polisi wamesema gari hilo lilikuwa katika mwendo
kasi mno.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni