Kocha Jose
Mourinho anayependa majigambo ameamua kumeza kiburi chake na kukiri
kuwa kwa mwenendo huu wa Chelsea unaoendelea katika Ligi Kuu ya
Uingereza watashindwa kutetea taji lao.
Katika kuonyesha
kuwa amechukizwa na matokeo ya timu yake Mourinho amesema alitamani
awatoe kuwabadilisha wachezaji sita katika mchezo wao na New Castle
ulioshia kwa sare ya bahati ya mabao 2-2.
Kocha Mourinho
amesema anakerwa na ufanisi duni wa wachezaji wake kama saba bila ya
kuwataja majina na kusema iwapo hali haitobadilika Chelsea si
itapoteza kombe bali itapoteza kila mechi.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni