Vyama vikuu
vinavyounga kupatikana kwa uhuru wa mkoa wa Catalonia kutoka Hispania
vimeshinda uchaguzi kwa mujibu wa matokeo yaliyotolewa.
Wakati kura
zipatazo asilimia 100 zikiwa zinahesabiwa muungano mkuu unaotaka
kujitenga na vyama vidogo umeshinda kwa viti 72 katika viti 135 vya
bunge la mkoa huo.
Wamesema ushindi
huo mkubwa utawapa fursa ya wao kujitangaza kujitenga na Hispania
katika kipindi cha miezi 18.
Serikali kuu ya
Hispania imeapa kupinga mahakamani hatua yoyote ya mkoa huo kutaka
kupatiwa uhuru.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni