.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Ijumaa, 18 Septemba 2015

KATIBU MKUU WA FIFA JEROME VALCKE ASIMAMISHWA WADHIFA WAKE

Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Duniani FIFA Jerome Valcke amesimamishwa kibarua chake hadi itakapotangazwa tena na kutokana na tuhuma za rushwa anazohusishwa nazo.

Taarifa iliyotolewa na FIFA imesema imekuwa ikifahamu mfululizo wa tuhuma zinazomkabili katibu huyo na inaendelea na uchunguzi kupitia kamati yake ya maadili.

Shutuma zilizoandikwa na gazeti moja siku yaAalhamisi zimedai kuwa Velcke amehusika na uuzaji wa tiketi za kombe la dunia kwa ghalama za juu.

Huo ni mwendelezo wa jinamizi lililoifika FIFA ambapo hadi sasa maafisa saba wa shirikisho hilo wapo lupango kwa tuhuma za rushwa, tangu mwezi Mei hali iliyopelekea Rais wa FIFA Sepp Blatter kutangaza kujiuzulu na kuitisha uchaguzi mwingine wa FIFA utakaofnyika Februari mwakani.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni