Golikipa wa timu ya Manchester
United ya Uingereza David De Gea ametia saini mkataba mpya wa miaka
minne na klabu hiyo.
Mchezaji huyo raia wa Hispania
mwenye umri wa miaka 24 alikaribia kujiunga na Real Madrid katika
siku ya mwisho ya uhamisho, hata hivyo ilishindikana kutokana na
nyaraka muhimu kutowasilishwa kwa wakati.
Mkataba wa De Gea wa awali ulikuwa
umalizike majira yajayo ya joto, ambapo mkataba mpya aliopewa unatoa
fursa kuongeza mwaka mwingine.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni