Jitihada za uokoaji zinaendelea eneo
la kaskazini mashariki mwa Japan, ambako watu wapatao watatu wamekufa
katika mafuriko makubwa na wengine wengi wamekwama.
Watu 24 hawajulikani walipo na
wengine 27 wamejeruhiwa nane kati yao wakiwa katika hali mbaya zaidi.
Maafisa wameonya kuwepo kwa mvua
kubwa na hatari ya kutokea maporomoko ya ardhi, wakati hali hiyo
mbaya ya hewa ikielekea eneo la kaskazini mwa Japan.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni