.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Alhamisi, 17 Septemba 2015

MAAFISA WA ULINZI WA RAIS WA BURKINA FASO WAFANYA MAPINDUZI NA KUTANGAZA KIONGOZI MPYA

Maafisa wa ulinzi wa rais nchini Burkina Faso wametwaa madaraka ya nchi katika mapinduzi, huku milio ya risasi ikiripotiwa kusikika katika Jiji la Ouagadougou.

Mtu wa karibu wa aliyekuwa rais wa nchi hiyo Blaise Compaore ametangazwa kuwa ndiye kiongozi mpya wa Burkina Faso katika televisheni ya taifa.

Rais wa Ufaransa Francois Hollande ameshutumu mapinduzi hayo katika taifa hilo ambalo lilikuwa ni koloni la Ufaransa.

Vikosi vya rais vimewafyatulia risasi waandamanaji ili kuwasambaza katika Jiji la Ouagadougou na baadhi yao wamekamatwa.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni