.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 16 Septemba 2015

MAKAMU WA RAIS AADHIMISHA KILELE CHA SIKU YA MARA (MARA DAY) BUTIAMA MKOANI MARA

3
Makamu wa Rais waJamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia wakati wa sherehe za maadhimisho ya Kilele cha Siku ya Mara (Mara Day) zilizofanyika kwenye Uwanja wa Mwitongo, Butiama mkoani Mara leo Sept 15, 2015. Picha zote na OMR
6
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Mbogo Futakamba (kushoto) na Waziri wa Maji na Umwagiliaji wa Kenya, Eugene Wamalwa (katikati) wakitiliana saini mkataba wa Maridhiano ya Mto Mara wakati wa sherehe za Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mara (Mara Day) zilizofanyika Butiama mkoani Mara leo Sept 15, 2015. Kulia ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanznia, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akishuhudia.
5
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Mbogo Futakamba (kushoto) akibadilishana mikataba na Waziri wa Maji na Umwagiliaji wa Kenya, Eugene Wamalwa, mara baada ya kusainiana Mkataba huo wa Maridhiano ya Mto Mara, wakati wa sherehe za Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mara (Mara Day) zilizofanyika Butiama mkoani Mara leo Sept 15, 2015. Kulia ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanznia, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akishuhudia.
7
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimkabidhi Tuzo ya kushiriki maadhimisho na kutunza mazingira, Mwakilishi wa Serikali ya Jimbo la Narok nchini Kenya, Rebeccah Seenoi, wakati wa sherehe za maadhimisho ya Kilele cha Siku ya Mara (Mara Day) zilizofanyika kwenye Uwanja wa Mwenge, Butiama mkoani Mara leo Sept 15, 2015.
8
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akipata maelezo kutoka kwa Eugene Muramira, wakati alipotembelea katika Banda la maonesho la Afrika Mashariki, wakati wa Sherehe za Maadhimisho ya Kilele cha Siku ya Mara (Mara Day) zilizofanyika leo Sept 15, 2015 kwenye Uwanja wa Mwenge Butiama Mkoani Mara.
9
1
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muugano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwasha Mshumaa katika Kaburi ya Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, kama ishara ya Kumbukumbu wakati alipofika katika Jumba la makumbusho Butiama mkoani Mara leo Sept 15, 2015 baadda ya kuadhimisha Kilele cha Siku ya Mara (Mara Day) iliyofanyika Butiama.
2
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muugano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiweka Shada la Maua katika Kaburi ya Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, kama ishara ya Kumbukumbu wakati alipofika katika Jumba la makumbusho Butiama mkoani Mara leo Sept 15, 2015 baadda ya kuadhimisha Kilele cha Siku ya Mara (Mara Day) iliyofanyika Butiama. Kushoto ni Waziri wa Maji na Umwagiliaji wa Kenya, Eugene Wamalwa.
13
11

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni