.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 27 Septemba 2015

MANCHESTER UNITED YAKAA KILELENI MWA LIGI KUU YA UINGEREZA

Timu ya Manchester United inamaliza wiki hii ikiwa kileleni mwa Ligi Kuu ya Uingereza kwa mara ya kwanza tangu kocha wao wa zamani Sir Alex Ferguson ajiuzulu mwaka 2013, baada ya jana kupata ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Sunderland.

Katika mchezo huo Memphis Depay, Wayne Rooney walifunga magoli yao yao ya kwanza katika Ligi Kuu ya Uingereza tangu mwezi April na kumaliza ukame wa magoli, huku Juan Mata naye akicheka na nyavu katika dakika za nyongeza.
                         Memphis Depay akifunga bao la kwanza kwa Manchester United 
Nayo Chelsea ililazimika kuamka kutoka usingizini baada ya kuduwazwa kwa mabao 2 na New Castle na kufanikiwa kuyachomoa yote kupitia Willian na Ramires na kumaliza mechi kwa sare ya mabao 2-2.
            Kocha wa Chelsea Jose Mourinho akionekana kutofurahishwa na matokeo
Arsenal nao wameibuka na ushindi mnono wa mabao 5-2 dhidi ya Leicester City, huku Alexis Sanchez akipachika mabao matatu peke yake yaani hat-trick, katika mchezo ambao walitanguliwa kufungwa.
Matokeo mengine ni Tottenham 4-1 Man City, Liverpool 3-2 Aston Villa, Southampton 3-1 Swansea, Stoke 2-1 Bournemouth na West Ham 2-2 Norwich.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni