.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumapili, 27 Septemba 2015

MWANAMUZIKI WA MAREKANI CHRIS BROWN HUENDA AKAZUILIWA KUTUMBUIZA AUSTRALIA

Mwanamuziki wa Marekani Chris Brown ameambiwa kuwa kunauwezekano wa kutopatiwa ruhusa kutumbuiza nchini Australia kutokana na rekodi yake ya ugomvi katika mahusiano.

Nyota huyo amepangiwa kufanya ziara ya muziki nchini Australia mwezi Desemba, na tiketi za shoo zake zinatarajiwa kuanza kuuzwa kuanzia kesho. Chris anasiku 28 za kupinga zuio hilo.

Mnamo mwaka 2009, Chris Brown alikiri kosa la kumpiga mpenzi wake wa zamani nyota wa pop Rihanna, na alishatembelea Australia mara mbili lakini sasa serikali inashinikizwa kumzuia.

Idara ya Uhamiaji ya Australia imetoa notisi ya kuonyesha nia ya kumyima kuingia nchi hiyo Chris Brown, Waziri wa Uhamiaji Peter Dutton amesema.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni