Mshambuliaji wa Manchester United
Memphis Depay ameonekana akiwa ameenda kufanya manunuzi madukani
nchini Uingereza akiwa na mwanamitindo Mmarekani Karrueche Tran.
Memphis Depay ameonekana jana na
Karrueche ambaye alikuwa ni mpenzi wa mwanamuziki Chris Brown na
kuanza kuibua minong'ono huenda wawili hao wameanzisha mahusiano ya
karibu.
Siku ya jumamosi pia Depay na
Karrueche walionekana katika vijiwe tofauti Uingereza ambapo
walipigwa picha wakiwa pamoja nje ya klabu za usiku za Suburbia na
Club LIV.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni