Mtoto wa kike wa nyota wa filamu za
Fast and the Furious marehemu Paul Walker anatarajia kuishtaki
kampuni ya kutengeneza magari ya Porsche kutokana na ajali
iliyosababisha kifo cha baba yake.
Walker alikuwa ni abiria katika gari
aina ya Porsche lililokuwa likiendeshwa na rafiki yake wakati
lilipogonga nguzo na kulipuka moto Novemba mwaka 2013 na kusababisha
vifo vyao.
Vyombo vya habari vya Marekani
vimeripoti kufunguliwa shitaka la kifo cha makosa na binti wa Walker
aitwae Meadow, kwa madai watengenezaji gari hilo hawakuzingatia
usalama wa waendeshaji.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni