Mwanafunzi wakike wa chuo mzaliwa wa
Tanzania, Mercy Bundi amejiuwa nchini Kenya kwa kunywa sumu baada ya
kuanzisha mahusiano ya mapenzi kwa njia ya Facebook na raia wa kigeni
ambayo yaliishia kuwa ya kumdhalilisha, vipigo na vitisho.
Marehemu Mercy mwenye umri wa miaka
19, ameacha ujumbe uliomtaja raia huyo wa kigeni Marco Ritz, ambaye
alimtishia kuwa atamshitaki atasambaza picha zake za utupu alizompiga
na kuieleza dunia kuwa yeye ni kahaba.
Katika waraka wake huo Mercy amesema
siku alipokutana na raia huyo wa kigeni ndipo maisha yake
yalipobadilika na kuwa ya matatizo kutokana na kupingwa,
kudhalilishwa pamoja na vitisho jambo liliomfanya afikie uamuzi wa
kujiua Septemba 12, mwaka huu.
Marehemu Mercy alianza elimu yake ya
msingi Kisii, akajiunga na Shule ya Wasichana ya Nyakach na baadae
kuhamia shule ya Sekondari ya Mtakatifu Michael huko Nakuru 2013,
mwaka huu alijiunga na Chuo cha Bugema, hadi alipojiua.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni