Polisi nchini Argentina
wamemfungulia mashtaka mwanaume mmoja ambaye anadaiwa kumfungia
kwenye chumba mkewe pamoja na mtoto wake mkubwa wa kiume kwa miaka
kadhaa kama wafungwa.
Polisi wamesema chumba hicho kichafu
chenye harufu mbaya kilichopo kwenye nyumba ya Bw. Edgardo Oviedo
katika mji wa pwani wa Mar del Plata kina mlango wa chuma na kufuli
kwa nje.
Pia , walikuta vyakula vya mbwa,
ambavyo inaaminika kuwa alikuwa akimpatia mkewe huyo na mtoto wake wa
kiume.
Polisi wamesema mkewe amekutwa na
matatizo ya akili na mtoto wake wa kiume mwenye umri wa miaka 33
hawezi hata kuzungumza.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni