.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatatu, 7 Septemba 2015

RAIS YOWERI MUSEVENI AWATAKA VIJANA KUTOPATA UJAUZITO KWA UZEMBE

Rais Yoweri Museveni wa Uganda amesema kitendo cha kupata watoto kwa uzembe na kutegemea wasamaria wema kuwaangalia kinachangia ongezeko la kuwapo kwa watoto ambao maisha yao yapo hatarini nchini humo.

Akiongea katika maadhimisho ya kumi ya kituo cha Watoto cha Kampala (KCC) kinachoangalia watoto waliohatarini, Rais Museveni ametaka kuwapo kwa nidhamu miongoni mwa raia wa Uganda ili kuepusha kile alichokiita kosa la kijamii.

Amewaasa watoto wa kituo hicho kutojitumbukiza katika masuala ya uzazi hadi hapo wakati muafaka utakapofika, na kuwasisitiza kutofanya ngono zembe jambo ambalo linaweza kuwafanya wapate maambukizi ya Ukimwi.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni