Robert Lewandowski
amefunga magoli matano ndani ya dakika tisa baada ya kuingia akitokea
benchi la Bayern Munich katika ushindi ulioweka historia katika Ligi
ya Kuu ya Ujerumani, Bundesliga dhidi ya Wolfsburg.
Bayern ilikuwa imelala kwa bao moja
kwa bila katika kipindi cha kwanza, kabla ya Lewandowski alipoingia
dimbani kuchukua nafasi ya Thiago katika kipindi cha pili na
kubadilisha matokeo ya mchezo huo kuwa 5-1.
Dakika sita tu kupita tangu aingie
uwanjani mchezaji huyo raia wa Poland alipachika wavuni bao la kwanza
na kuongeza mengine manne na kuweka rekodi ya mabao matano
yaliyofungwa haraka na mchezaji mmoja katika historia ya Bundesliga.
Robert Lewandowski akipachika bao la tatu
Kocha Pep Guardiola akishika kichwa asiamini alichofanya Lewandowski
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni