Mchezaji mtukutu Mario Balotelli
amefunga goli lake la kwanza tangu ajiunge na AC Milan na kuizamisha
timu ya Udinese ambayo imeporomoka hadi katika kundi la kushuka
daraja kufuatia kupoteza mechi nne mfululizo.
Mchezaji huyo wa Liverpool ambaye
anachezea AC Milan kwa mkopo alifunga goli la kwanza kwa mkwaju murwa
wa adhabu, wakati timu yake ikiibuka na ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya
Udinise.
Mabao mengine ya AC Milani
yalipachikiwa kimiani na Giacomo Bonaventura pamoja na Cristian
Zapata aliyepachika wavuni bao la mpira wa kichwa katika mchezo huo
wa Ligi Kuu ya Italia.


Hakuna maoni :
Chapisha Maoni