Serikali imefuta hati miliki ya
mashamba makubwa manne, badala yake wananchi wenye uhaba wa ardhi
waliojiorodhesha kutokana na migogoro hiyo, watapewa ardhi kwa
kupimiwa maeneo yao .
Aidha Mashamba yaliyofutiwa hati
miliki hiyo ni Tanzania Plantations Limited, pamoja Shamba la Noors
lililopo kijiji cha Laroi na kisima cha mungu huko Oljoro.
Kuchukuliwa kwa mashamba hayo na
serikali ni kuondoa mgogoro wa muda mrefu uliokuwa unasababisha
mapigano ya mara kwa mara na uvamizi wa mashamba na wananchi hao, kwa
kudai ardhi iliyokuwa inamilikiwa na wawekezaji hao bila kuendelezwa.
Akizungumza leo Jijini hapa
,Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi,
amesema serikali imeamua kufuta miliki ya mashamba hayo, ili kuwapa
wananchi waweze kugaiwa kihalali na kupimiwa maeneo yao kwa watu
ambao hawana ardhi ambao walianishwa hapo awali.
Ameyataja mashamba yaliyofutiwa
hati hizo na Rais ni Tanzania Plantion yenye namba lenye hati NP
305,NP 304 na C.T.No 5189 yenye ukubwa wa ekari 6,396 na ni mali ya
serikali na stahili ya mwekezaji huyo ni fidia.
Lakini pia katika ufutaji wa
mashamba hayo mwekezaji amebakiziwa shamba lenye namba N.371 ambalo
analimiliki kihalali lakini kwamakubaliano na serikali ameamua kutoa
heka 100 kwaajili ya
kuwasaidia wananchi wenye uhaba wa
ardhi na kilimo katika Halmashauri ya Meru.
Amesema baada ya ubatilishaji wa
mashamba ya Tanzania Plantion Ltd pamoja na ardhi aliyoitoa mwekezaji
huyo kwa hiari yake Halmashauri ya Wilaya ya Arusha imepata jumla ya
ekari 6176.5na Halmahauru ya Meru ekari 925.
Lukuvi amesema Wananchi zaidi ya
2000 watapata maeneo ya kujenga (makazi) na kilimo lakini alisisitiza
kazi hiyo itasimamiwa na timu ya wataalam, iliyoundwa kwaajili ya
kusimamia ugawaji wa maeneo hayo kwa wananchi wenye uhaba wa ardhi.
Aidha amesema wiki iliyopita
mashamba zaidi ya 7 Wilayani Mvumero yalifutiwa ulimiliki wa ardhi,10
Wilayani Kibaha Mkoani Pwani na hivi mashamba ya watu wakubwa 10
yaliyopo Kilombero Mkoani Mgogoro yatafutwa hati miliki zake, kwani
haiwezekani matajiri kula kuku mjini wakiyatelekeza na wengine
kukodisha wananchi wazawa kuyalima huku wananchi hao wakiwa hawana
ardhi.
Wakati huo huo serikali imefuta hati
miliki za mashamba 48, zilizokuwa zinamilikiwa na wawekezaji
wilayani Monduli na kuleta kero ya mara kwa mara kwa wananchi pia
kwa mkoa wa Manyara Rais amefuta shamba la Ufyomi Gallapo Estate,
lenye ekari 120 ili kufidia wananchi 340 waliohamishwa kupisha
Hifadhi ya Tarangire.
Mwisho

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni