Serikali ya Ugiriki na Maafisa wa
Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuwahudumia Wakimbizi wameongeza
wafanyakazi zaidi pamoja na meli za kuwachukua wahamiaji 25,000
waliokwama kwenye kisiwa cha Lesbos.
Kituo cha kuorodhesha wahamiaji
kimewekwa kwenye uwanja wa mpira uliotelekezwa ili kuwasaidia
wahamiaji kwenda Jijini Athens nchini Ugiriki.
Wakati huo huo maelfu ya wahamiaji
wamevunja uzio wa polisi katika mpaka wa Hangari na Serbia na
kutembea kuelekea Jiji la Budapest.

Hakuna maoni :
Chapisha Maoni