.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumanne, 8 Septemba 2015

WAZAZI WALIOBADILISHIWA MTOTO WAUNGANISHWA NAE BAADA YA KUPATIKANA



Wazazi raia wa Uingereza wameunganishwa na mtoto wao mchanga wa kiume baada ya kumtuhumu daktari mmoja wa El Salvador kwa kuwabadilishia mtoto wao wa kiume baada ya kujifungua.

Wazazi hao Richard Cushworth pamoja na mkewe raia wa Salvador, Mercedes Casanella wamesema walikuwa wahanga wa tukio la usafirishaji watoto.

Jaji nchini El Salvador aliagiza kurejeshewa mtoto wao halisi wazazi hao baada ya kufanyika vipimo vya kubaini vinasaba vya DNA, ikiwa ni miezi minne kupita baada ya kuzaliwa mtoto huyo.

Daktari huyo aliyekanusha kufanya kosa lolote, anachunguzwa na mamlaka za EL Salvador.
              Richard Cushworth na mkewe Mercedes Casanella wakiwa na mtoto waliobambikiwa
                      Mama Cushworth akiwa na mtoto wake halisi baada ya kujifungua

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni