.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 23 Septemba 2015

UMOJA WA ULAYA WAELEKEA KURIDHIA MPANGO WA LAZIMA WA KUGAWANA WAHAMIAJI

Viongozi wa Umoja wa Ulaya (EU) Jijini Brussels wanajipanga kuridhia mpango wa kugawana wahamiaji 120,000 katika bara hilo, licha ya upinzani mkali kutoka kwa wanachama.

Nchi za Romania, Jamhuri ya Czech Republic, Slovakia na Hangari zilipiga kura kupinga mgawano wa lazima wa wahamiaji hao kwa nchi wanachama wa EU.

Mkutano wa hii leo pia utajadili juu ya kuongeza udhibiti wa mipaka ya mataifa ya Umoja wa Ulaya, na kuongeza misaada kwa mataifa jirani na Syria ambayo ndiyo inayozalisha wahamiaji wengi.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni