Wachezaji wa West Ham Victor Moses
na Diafra Sakho wameitibuliwa Manchester City kasi yake ya ushindi wa
mfululizo katika Ligi kuu ya Uingereza baada ya kuiduwaza nyumbani
kwa mabao 2-1.
Katika mchezo huo uliochezwa kwenye
dimba la Etihad Victor Moses anayeichezea West Ham kwa mkopo
alipachika bao la kwanza kwa shuti la umbali wa yadi 20, mnamo dakika
ya sita tu ya mchezo.
Bao la pili la West Ham lilipachikwa
kimiani na Diafra Sakho, huku bao pekee la Manchester City
likipachikiwa kimiani na Kevin De Bruyne likiwa ni bao lake la kwanza
tangu ajiunge na timu hiyo.
Diafra Sakho akimpoteza kipa Hart wa Manchester City na kupachika bao
Victor Moses akiruka juu kufurahi bao lake alilofunga
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni