Kocha Arsene Wenger amelisihi
Shirikisho la Soka la Uingereza kumfungia mechi tatu Diego Costa, na
kumshutumu refa Mike Dean kwa kushindwa kumudu mchezo wao ambao
mshambuliaji huyo wa Chelsea akichangia ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya
Arsenal.
Wenger alikera na kitendo cha Costa
kutoadhibiwa na refa baada ya kumzaba kofi Laurent Koscielny na
kumsukuma chini kabla ya mapumziko na kulazimika beki wa Arsenal
Gabriel kutolewa nje wakati alipokerwa na kitendo cha Costa na
kulipiza kwa kumpiga teke la nyuma.
Wenger amekiri kuwa mchezaji wake
Gabriel alipaswa kutolewa nje, hata hivyo amemtupia lawama refa kwa
kuonyesha udhaifu wa kumuachia Costa kufanya makosa bila kumpa
adhabu, na kuongeza kuwa wameshangazwa na kiwango cha refa Mike Dean.
Beki wa Arsenal Gabriel akizuiliwa asiende kugombana na Diego Costa
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni