.

.

.

.

.

.

.

.
KARIBUNI TUHABARIKE, TUELIMISHANE, TUPEANE HABARI ZA KUKUFANYA UTABASAMU KIDOGO NA MATUKIO YALIYOFANYIWA UCHUNGUZI WA KINA TOKA KILA PEMBE CONTACTS: +255 787 377 722 Email: drweyunga@gmail.com PIA UNAWEZA KUNI FOLLOW KUPITIA INSTAGRAM YANGU @drweyunga | TANGAZA NASI ILI UWAFIKIE WATU WENGI ZAIDI.

Jumatano, 2 Septemba 2015

WAHAMIAJI WABUNI KILA NJIA ILIMRADI TU WAINGIE BARA LA ULAYA

Wahamiaji wawili kutoka nchi za Afrika Magharibi, wameingia eneo la Hispania la Ceuta wakitokea Morocco wakiwa wamejichimbia kwenye eneo la injini ya gari na nyuma ya kiti cha nyuma cha gari aina ya Mercedes-300.

Polisi nchini Hispania iliwabaini watu hao siku ya jumapili wakati maafisa forodha wakifanya ukaguzi katika mpaka wa El Tarajal, karibu na mpaka wa Moroccan.

Wahamiaji hao wawili wote wanaume wanatokea Guinea walipatiwa huduma ya kwanza kutokana na kukosa hewa ya oxygen, maafisa polisi wa eneo la Guardia nchini Hispania wamesema.
                                                  Mhamiaji akiwa amejificha eneo la injini ya gari
                                              Huyu mwingine alikutwa nyuma ya kiti cha gari

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni